Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yoshua 18:25 - Swahili Revised Union Version

25 na Gibeoni, na Rama, na Beerothi;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

25 Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

25 Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

25 Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

25 Gibeoni, Rama na Beerothi,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

25 Gibeoni, Rama na Beerothi,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

25 na Gibeoni, na Rama, na Beerothi;

Tazama sura Nakili




Yoshua 18:25
25 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Abneri, mwana wa Neri, na watumishi wa Ishboshethi, mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.


Na huyo mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili, viongozi wa vikosi; jina lake mmoja akiitwa Baana, na jina la wa pili Rekabu wana wa Rimoni, Mbeerothi, wa wana wa Benyamini; (kwa maana Beerothi umehesabiwa kuwa wa Benyamini;


Kisha, Baasha mfalme wa Israeli akashambulia Yuda, akaujenga Rama, ili asimwache mtu yeyote kutoka wala kuingia kwa Asa mfalme wa Yuda.


basi, BWANA akamtokea Sulemani mara ya pili kama alivyomtokea huko Gibeoni.


Basi huko Gibea alikaa babaye Gibea, jina lake Yeieli, ambaye jina la mkewe aliitwa Maaka;


Watu wa Rama na Geba, mia sita ishirini na mmoja.


Hazori, Rama, Gitaimu;


wamevuka kivuko; wamekwenda kulala katika Geba; Rama unatetemeka; Gibea wa Sauli umekimbia.


Maana BWANA ataondoka kama vile katika mlima Perasimu, ataghadhibika kama vile katika bonde la Gibeoni; apate kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu; na kulitimiza tendo lake, tendo lake la ajabu.


BWANA asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako.


Na ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;


ndipo wakaogopa mno, kwa sababu Gibeoni ulikuwa ni mji mkubwa, kama ilivyo miji ya kifalme mmojawapo, tena kwa sababu ulikuwa ni mji mkubwa kupita Ai, tena watu wake wote walikuwa ni mashujaa.


Zanoa, Enganimu, Tapua, Enamu;


na Kefar-amoni, na Ofni, na Geba; miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake;


na Mispa, na Kefira, na Moza;


kisha mpaka ulizunguka kuelekea Rama, na mji wa Tiro ulio na boma; kisha mpaka ulizunguka kuelekea Hosa; na matokeo yake yalikuwa baharini katika nchi ya Akzibu;


Tena katika kabila la Benyamini, Gibeoni pamoja na mbuga zake za malisho, na Geba pamoja na mbuga zake za malisho;


Akazisongeza jamaa za Yuda, akaitwaa jamaa ya Wazera; akaisongeza jamaa ya Wazera mtu kwa mtu; Zabdi akatwaliwa.


Kisha wana wa Israeli walisafiri, wakaifikia miji ya watu hao siku ya tatu. Basi miji ya watu hao ilikuwa ni hii, Gibeoni, na Kefira, na Beerothi, na Kiriath-yearimu.


Lakini wenyeji wa Gibeoni waliposikia habari ya hayo yote Yoshua aliyokuwa amewatenda watu wa Yeriko, na wa Ai,


Bwana wake akamwambia, Hatutageuka sisi kuingia mji wa wageni, ambao si wa wana wa Israeli; lakini tutapita mpaka Gibea.


Kisha akamwambia mtumishi wake, Haya, tuifikie miji hii mmojawapo nasi tutalala katika Gibea au katika Rama.


Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu


Wakaondoka asubuhi na mapema, wakaomba mbele za BWANA, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye BWANA akamkumbuka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo