Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yohana 10:27 - Swahili Revised Union Version

27 Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

27 Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.

Tazama sura Nakili




Yohana 10:27
26 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasitasita katikati ya mawazo mawili hata lini? BWANA akiwa ndiye Mungu, mfuateni; bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno.


Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema BWANA, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa.


Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.


Alipokuwa bado akisema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.


Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.


Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.


Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Nenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.


Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu yeyote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.


Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.


Akawaambia wote, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.


Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;


Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.


Wote walionitangulia ni wezi na wanyang'anyi; lakini kondoo hawakuwasikia.


Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.


Yesu akamwambia, Ikiwa nataka huyu akae hata nitakapokuja, imekuhusuje wewe? Wewe unifuate mimi.


Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.


Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.


Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamuwezi kulisikia neno langu.


Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake.


Lakini mtu akimpenda Mungu, huyo amejulikana naye.


Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena?


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mkisikia sauti yake,


Hawa ndio wasiojitia unajisi na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio wamfuatao Mwana-kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-kondoo.


Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo