Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yoeli 1:10 - Swahili Revised Union Version

10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Mashamba yamebaki matupu; nchi inaomboleza, maana nafaka imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Mashamba yamebaki matupu; nchi inaomboleza, maana nafaka imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Mashamba yamebaki matupu; nchi inaomboleza, maana nafaka imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Mashamba yameharibiwa, ardhi imekauka; nafaka imeharibiwa, mvinyo mpya umekauka, mafuta yamekoma.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Mashamba yameharibiwa, ardhi imekauka; nafaka imeharibiwa, mvinyo mpya umekauka, mafuta yamekoma.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka.

Tazama sura Nakili




Yoeli 1:10
19 Marejeleo ya Msalaba  

utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na makao duniani.


Kwa maana maji ya Nimrimu yamekuwa mahali palipoharibika, kwa kuwa majani yamekauka, miche imenyauka, majani mabichi yamekoma.


Pana kilio katika njia kuu kwa sababu ya divai; furaha yote imetiwa giza, na changamko la nchi limetoweka.


Divai mpya inaomboleza, mzabibu umedhoofika, watu wote waliochangamka moyo wanaugua.


Wamelifanya kuwa ukiwa, na kwa kuwa ni ukiwa linanililia; nchi yote imefanywa kuwa ukiwa, kwa sababu hapana mtu aliyeweka haya moyoni mwake.


Hata lini itaomboleza nchi, na kukauka majani ya nchi yote? Kwa ajili ya mabaya yao wakaao ndani yake, wanyama wameangamia na ndege pia; kwa sababu walisema, Yu kipofu katika njia zetu.


Furaha na shangwe zimeondoshwa, katika shamba lizaalo sana, na katika nchi ya Moabu; nami nimeikomesha divai katika mashinikizo; hapana mtu atakayekanyaga zabibu kwa shangwe; shangwe ile itakuwa si shangwe.


Kwa ajili ya hayo nchi itaomboleza, na kila mtu akaaye ndani yake atadhoofika, pamoja na wanyama wa porini na ndege wa angani; naam, samaki wa baharini pia wataangamizwa.


Sakafu na shinikizo hazitawalisha, na divai mpya itampungukia.


Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imetoweka kwa wanadamu.


Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.


BWANA akajibu, akawaambia watu wake; Tazameni, nitawaletea nafaka, na divai, na mafuta, nanyi mtashiba kwa vitu hivyo; wala sitawafanya tena kuwa aibu kati ya mataifa;


na nguvu zenu mtazitumia bure; kwa kuwa nchi yenu haitazaa mazao yake, wala miti ya nchi haitazaa matunda yake.


Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula; Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe;


Nami nikaita wakati wa joto uje juu ya nchi, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya, na juu ya mafuta, na juu ya kila kitu itoacho nchi, na juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya kazi zote za mikono.


Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo


Tufuate:

Matangazo


Matangazo