Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 6:10 - Swahili Revised Union Version

10 Hapo ndipo ningefarijika hata sasa; Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha; Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Hiyo ingekuwa faraja yangu, ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Hiyo ingekuwa faraja yangu, ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Hiyo ingekuwa faraja yangu, ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.

Tazama sura Nakili




Yobu 6:10
27 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi, Nami ni safi machoni pako.


Je! Utulivu wa Mungu ni mdogo sana kwako, Maliwazo ya Mungu ni madogo sana kwako?


Udongo wa bondeni utakuwa tamu kwake, Na watu wote watafuata nyuma yake, Kama vile walivyomtangulia watu wasiohesabika.


Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako.


Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.


Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,


Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi?


Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu; Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?


Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.


Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenipa moyo.


Kinywa chake mwenye haki hunena hekima, Na ulimi wake husema hukumu.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Sitatumia ukali wa hasira yangu, sitamwangamiza Efraimu tena; kwa maana mimi ni Mungu, si mwanadamu mimi; mimi ndiye aliye Mtakatifu katikati yenu; wala sitaingia ndani ya mji.


Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli, uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wenu, ni mtakatifu.


Ee BWANA, Mungu wangu, mtakatifu wangu, wewe si wa milele? Hatutakufa. Ee BWANA, umemwandikia hukumu, nawe, Ee Jabali, umemweka imara ili aadhibishwe.


Mungu alikuja kutoka Temani, Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani. Utukufu wake ukazifunika mbingu, Nayo dunia ikajaa sifa yake.


ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lolote liwezalo kuwafaa bali niliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba,


Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.


Yeye ambaye hakumhurumia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje pia kutupa chochote kingine pamoja naye?


BWANA hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya BWANA na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA atalifuta jina lake chini ya mbingu.


Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.


Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja.


Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA; Kwa maana hakuna yeyote ila wewe, Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo