Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 4:3 - Swahili Revised Union Version

3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi, Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi, na kuiimarisha mikono ya wanyonge.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi, na kuiimarisha mikono ya wanyonge.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi, na kuiimarisha mikono ya wanyonge.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Fikiri jinsi umewafundisha watu wengi, jinsi umeitia nguvu mikono iliyokuwa dhaifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Fikiri jinsi ambavyo umewafundisha watu wengi, jinsi ambavyo umeitia nguvu mikono iliyokuwa dhaifu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi, Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.

Tazama sura Nakili




Yobu 4:3
21 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana nimemchagua ili awaamuru wanawe na vizazi vyake baada yake wadumishe njia ya BWANA, kwa kuwa wenye haki na kweli, ili BWANA naye akamtimizie Abrahamu ahadi zake.


wakaifanya sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu kwa furaha, kwa muda wa siku saba; kwa kuwa BWANA amewafurahisha, na kumgeuza moyo mfalme wa Ashuru, awaelekee, ili awatie nguvu mikono yao katika kazi hiyo ya nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.


Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu, Na maliwazo ya midomo yangu yangewatuliza.


Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia.


Nilikuwa macho kwa kipofu, Nilikuwa miguu kwa aliyechechemea.


Nilikuwa baba kwa mhitaji, Na kesi ya mtu nisiyemjua niliichunguza.


Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja, Wakanyamaza kimya wapate kusikia mashauri yangu.


Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka, Nawe umeyaimarisha magoti manyonge.


Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi; Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.


Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.


Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara; Utamu wa maneno huongeza elimu.


Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu, yaimarisheni magoti yaliyolegea.


Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.


Kwa kuwa ninyi mmemhuzunisha moyo mwenye haki kwa uongo, ambaye mimi sikumhuzunisha; na kuitia nguvu mikono ya mtu mbaya, hata asigeuke, na kuiacha njia yake mbaya, na kuhifadhika;


Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa, Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee.


lakini nimekuombea wewe ili imani yako isipungue; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.


Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.


Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.


Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na nguvu, umtie na nguvu; kwani ndiye atakayevuka mbele ya watu hawa, na nchi utakayoiona atawarithisha yeye.


Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolezwa chumvi, ili mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.


Kwa hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo