Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 10:9 - Swahili Revised Union Version

9 Kumbuka, nakusihi ulivyonifinyanga kama vile udongo; Nawe, je! Utanirudisha uvumbini tena?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Je, utanirudisha tena mavumbini?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Je, utanirudisha tena mavumbini?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo. Je, utanirudisha tena mavumbini?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

9 Kumbuka, nakusihi ulivyonifinyanga kama vile udongo; Nawe, je! Utanirudisha uvumbini tena?

Tazama sura Nakili




Yobu 10:9
25 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa kiumbe hai.


kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.


Je! Wewe hukunimimina kama maziwa, Na kunigandisha mfano wa jibini?


Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na dada yangu;


Tazama, mimi ni mbele ya Mungu kama ulivyo wewe; Mimi nami nilifinyangwa katika udongo.


Wenye mwili wote wangeangamia pamoja, Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.


Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo, Ambazo misingi yao i katika mchanga, Hao wanaopondwa kama nondo!


Nawe, je! Mbona hunisamehe makosa yangu, Na kuniondolea maovu yangu? Kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; Nawe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwapo.


Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo; Jicho langu halitaona mema tena.


Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.


Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao,


Ee BWANA, unikumbuke mimi, Kwa kibali ulicho nacho kwa watu wako. Unijie kwa wokovu wako,


Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti


Utazame mateso yangu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote.


Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.


Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!


Wamrudisha mtu mavumbini, usemapo, Rudini, enyi wanadamu.


Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.


Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unatengeneza nini? Au chombo ulichotengeneza hakina mikono?


Tena hapana aliitiaye jina lako, ajitahidiye akushike; kwa kuwa umetuficha uso wako, nawe umetukomesha kwa njia ya maovu yetu.


Lakini sasa, Ee BWANA, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.


Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema BWANA. Angalieni, kama udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo ninyi katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.


Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?


Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo