Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 9:5 - Swahili Revised Union Version

5 Nao watadanganya kila mtu jirani yake, wala hawatasema kweli; wameuzoesha ulimi wao kusema uongo; hujidhoofisha ili kutenda uovu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Kila mmoja humdanganya jirani yake, hakuna hata mmoja asemaye ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Kila mmoja humdanganya jirani yake, hakuna hata mmoja asemaye ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Kila mmoja humdanganya jirani yake, hakuna hata mmoja asemaye ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 Nao watadanganya kila mtu jirani yake, wala hawatasema kweli; wameuzoesha ulimi wao kusema uongo; hujidhoofisha ili kutenda uovu.

Tazama sura Nakili




Yeremia 9:5
32 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakashindwa kuupata mlango.


Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?


Kwani uovu wako unakufundisha kinywa chako, Nawe wachagua ulimi wake mwenye hila.


Wamenoa ndimi zao na kuwa kama za nyoka, Na katika midomo yao mna sumu ya fira.


Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako unatunga uongo.


Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.


Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wanaoyalenga maneno ya uchungu kama mishale,


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.


Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.


Ole wao wavutao uovu kwa kamba za ubatili, na dhambi kama kwa kamba za gari!


Ulikuwa umechoka kwa ajili ya urefu wa njia yako; lakini hukusema, Hapana matumaini; ulipata kuhuishwa nguvu zako; kwa sababu hiyo hukuugua.


Wamepanda ngano, lakini watavuna miiba; wamejiumiza nafsi zao, lakini hawatakuwa na faida; naam, tahayarini kwa ajili ya matunda yenu, kwa sababu ya hasira kali ya BWANA.


Kwa maana hata ndugu zako, na nyumba ya baba yako, wamekutenda mambo ya hila; naam, wamepiga kelele nyuma yako; usiwasadiki, wajapokuambia maneno mazuri.


Je! Mkushi aweza kuibadili ngozi yake, au chui madoadoa yake? Kama aweza, ndipo na ninyi mwaweza kutenda mema, ninyi mliozoea kutenda mabaya.


Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.


BWANA wa majeshi asema hivi, Kuta pana za Babeli zitabomolewa kabisa, na malango yake marefu yatateketezwa; nao watu watajitaabisha kwa ubatili, na mataifa kwa moto; nao watachoka.


nawe utasema, Hivyo ndivyo utakavyozama Babeli, wala hautazuka tena, kwa sababu ya mabaya yote nitakayoleta juu yake; nao watachoka. Maneno ya Yeremia yamefika hata hapa.


Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya BWANA, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali na vinywa vyao.


Huupinda ulimi wao, kana kwamba ni upinde, ili kusema uongo; nao wamepata nguvu katika nchi, lakini si katika uaminifu; maana huendelea toka ubaya hata ubaya, wala hawanijui mimi, asema BWANA.


Ulimi wao ni mshale ufishao; husema maneno ya hadaa; mtu mmoja husema maneno ya amani na mwenzake kwa kinywa chake, lakini moyoni mwake humwotea.


Amejidhoofisha kwa taabu, lakini kutu yake nyingi haikumtoka; kutu yake haitoki kwa moto.


Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri, na wenyeji wake wamesema uongo, na ulimi wao una udanganyifu kichwani mwao.


Enyi watu wangu, nimewatenda nini? Nami nimewachosha kwa kitu gani? Shuhudieni juu yangu.


Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa BWANA wa majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya ubatili?


Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu?


Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake.


kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;


Tena watu wote wa kizazi hicho nao walikusanywa waende kwa baba zao; kikainuka kizazi kingine nyuma yao, ambacho hakikumjua BWANA, wala hawakuijua hiyo kazi ambayo alikuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo