Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 12:6 - Swahili Revised Union Version

6 Kwa maana hata ndugu zako, na nyumba ya baba yako, wamekutenda mambo ya hila; naam, wamepiga kelele nyuma yako; usiwasadiki, wajapokuambia maneno mazuri.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Hata ndugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao pia wamekutendea mambo ya hila; wanakukemea waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, japo wanakuambia maneno mazuri.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Hata ndugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao pia wamekutendea mambo ya hila; wanakukemea waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, japo wanakuambia maneno mazuri.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Hata ndugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao pia wamekutendea mambo ya hila; wanakukemea waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, japo wanakuambia maneno mazuri.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Ndugu zako na jamaa zako nao wamekusaliti, wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini hata wakisema mema juu yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.

Tazama sura Nakili




Yeremia 12:6
25 Marejeleo ya Msalaba  

Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.


Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;


BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza, Na ulimi unenao maneno ya kiburi;


Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na asiyetambuliwa na wana wa mama yangu.


Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.


Anenapo maneno mazuri usimsadiki; Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.


Maana BWANA aniambia hivi, Kama vile ilivyo simba angurumapo na mwanasimba juu ya mawindo yake, wachungaji wengi wakiitwa ili kumpiga, lakini hatiwi hofu na sauti zao, wala kufanya woga kwa sababu ya mshindo wao; ndivyo BWANA wa majeshi atakavyoshuka ili kufanya vita juu ya mlima Sayuni, na juu ya kilima chake.


Lakini mimi nilikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.


Basi, kwa hiyo, BWANA asema hivi, juu ya watu wa Anathothi, watakao uhai wako, wakisema, Hutafanya unabii kwa jina la BWANA, usije ukafa kwa mkono wetu.


Maana nimesikia shutuma za watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.


Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa jangwani, kibanda cha wasafiri; nipate kuwaacha watu wangu, na kuondoka kwao! Maana wao ni wazinzi, wote pia, mkutano wa watu wenye hiana.


Huupinda ulimi wao, kana kwamba ni upinde, ili kusema uongo; nao wamepata nguvu katika nchi, lakini si katika uaminifu; maana huendelea toka ubaya hata ubaya, wala hawanijui mimi, asema BWANA.


Jihadharini, kila mtu na jirani yake, wala msimtumaini ndugu awaye yote; maana kila ndugu atachongea, na kila jirani atakwenda huku na huko na kusingizia.


Nao watadanganya kila mtu jirani yake, wala hawatasema kweli; wameuzoesha ulimi wao kusema uongo; hujidhoofisha ili kutenda uovu.


Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwaua.


Nao wakataka kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.


Maana hata nduguze hawakumwamini.


Makutano wote wakaondoka wakawaendea, mahakimu wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora.


Hata Galio alipokuwa mtawala wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya kiti cha hukumu,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo