Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waefeso 6:1 - Swahili Revised Union Version

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana Isa, kwa kuwa hili ni jema.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana Isa, kwa kuwa hili ni jema.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

Tazama sura Nakili




Waefeso 6:1
33 Marejeleo ya Msalaba  

na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu.


Israeli akamwambia Yusufu, Je! Ndugu zako hawachungi kondoo katika Shekemu? Njoo, nikutume kwao. Akamwambia, Mimi hapa.


Yusufu akawatoa katika magoti yake, naye akainama kifudifudi


Wanawe wakamfanyia kama alivyowaagiza;


Tena ulishuka juu ya mlima Sinai, ukasema nao toka mbinguni, ukawapa hukumu za haki, na sheria za kweli, na amri nzuri na maagizo;


Esta alikuwa hajadhihirisha jamaa yake wala kabila yake, kama vile Mordekai alivyomwagiza; kwa maana Esta alikuwa akiyashika maagizo ya Mordekai, vile vile kama wakati alipolelewa naye.


Yeye huimba mbele ya watu, na kusema, Mimi nimefanya dhambi, na kuyapotosha hayo yaliyoelekea, Wala sikulipizwa jambo hilo;


Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.


Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee BWANA, na kwa uaminifu umenitesa.


Maagizo ya BWANA ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya BWANA ni safi, Huyatia macho nuru.


Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,


Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.


Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao.


Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.


Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako.


Maneno ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, aliyowaamuru wanawe, kwamba wasinywe divai, yametimizwa, na hata leo hawanywi; maana wanaitii hiyo amri ya baba yao; lakini mimi nimesema nanyi, nikiamka mapema na kunena, bali ninyi hamkunisikiliza mimi.


Naye Yeremia akawaambia watu wa nyumba ya Warekabi, BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa sababu mmeitii amri ya Yonadabu, baba yenu, na kuyashika maagizo yake yote, na kutenda sawasawa na yote aliyowaamuru;


Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;


Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za BWANA zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.


Kila mtu na amche mama yake, na baba yake, nanyi mtazitunza Sabato zangu; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.


Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.


ili mmpokee katika Bwana, kama iwapasavyo watakatifu; mkamsaidie katika neno lolote atakalohitaji kwenu; kwa sababu yeye naye amekuwa msaidizi wa watu wengi, akanisaidia mimi pia.


Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.


Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mnajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.


Mtu akiwa na mwana mkaidi, mshupavu, asiyetii sauti ya baba yake, wala sauti ya mama yake, nao wajapomwadhibu hawasikizi,


Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.


Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; iwe ni mfalme kama mwenye cheo kikubwa;


Akamwambia, Hayo yote unenayo mimi nitayafanya.


Daudi akaondoka asubuhi na mapema, akawaacha kondoo pamoja na mchungaji, akavitwaa vitu vile, akaenda, kama Yese alivyomwamuru; akafika penye magari, wakati lile jeshi walipokuwa wakitoka kwenda kupigana, wakipiga kelele za vita.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo