Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waefeso 5:17 - Swahili Revised Union Version

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana Isa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana Isa.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Tazama sura Nakili




Waefeso 5:17
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu.


Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima, Wote wafanyao hayo wana ufahamu mzuri, Sifa zake zadumu milele.


Unifahamishe njia ya maagizo yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.


Akili za mwenye busara ni kujua njia yake; Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.


Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, Na kupata kumjua Mungu.


Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.


Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.


Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.


Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.


Basi angalieni sana jinsi mnavyoenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;


Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili.


Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;


Nendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.


shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.


Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo