Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Waebrania 10:4 - Swahili Revised Union Version

4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Tazama sura Nakili




Waebrania 10:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Maana hupendezwi na dhabihu, na kama ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.


Yeye achinjaye ng'ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.


Yafaa nini niletewe ubani kutoka Sheba, na udi kutoka nchi iliyo mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa hazikubaliwi, wala dhabihu zenu haziniridhii.


Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie BWANA; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng'ombe.


Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.


na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhabihu zote pia.


Kesho yake alimwona Yesu akija kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!


Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.


Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wowote kuwakamilisha wakaribiao.


Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.


Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),


ambayo ndiyo mfano wa wakati huu ulioko sasa; wakati huo sadaka na dhabihu zinatolewa, zisizoweza kwa jinsi ya dhambi kumkamilisha mtu aabuduye,


Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo