Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nehemia 9:35 - Swahili Revised Union Version

35 Kwa kuwa hawakukutumikia wewe katika ufalme wao, na katika wema wako mkuu uliowapa, na katika nchi ile kubwa yenye neema uliyowapa mbele yao, wala hawakubadili nia na kuyaacha mabaya yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

35 Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipoyafurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

35 Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipoyafurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

35 Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipoyafurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

35 Kwa kuwa hawakukutumikia wewe katika ufalme wao, na katika wema wako mkuu uliowapa, na katika nchi ile kubwa yenye neema uliyowapa mbele yao, wala hawakubadili nia na kuyaacha mabaya yao.

Tazama sura Nakili




Nehemia 9:35
11 Marejeleo ya Msalaba  

Wakaitwaa miji yenye ngome, na nchi yenye utajiri, wakazitamalaki nyumba zilizojaa vitu vyema, visima vilivyochimbwa, mizabibu, na mizeituni, na miti mingi yenye matunda; hivyo wakala, wakashiba, wakanenepa, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.


na wafalme wetu, na wakuu wetu, na makuhani wetu, na baba zetu, hawakuishika sheria yako, wala hawakuzisikiliza amri zako na shuhuda zako, ulizowashuhudia.


Nitautaja wema wa BWANA, sifa za BWANA kwa yote aliyotukirimia BWANA; na wingi wa wema wake kwa nyumba ya Israeli, aliowakirimia kwa rehema zake, na kwa wingi wa wema wake.


Tena itakuwa mtakapouliza, BWANA ametutenda mambo hayo yote kwa sababu gani? Ndipo utakapowaambia, Vile vile kama ninyi mlivyoniacha mimi, na kuwatumikia miungu mingine katika nchi yenu wenyewe, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi isiyo yenu.


Nao umeasi amri zangu, kwa kutenda mabaya kuliko mataifa hayo, nao umeasi sheria kuliko nchi hizo ziuzungukazo; maana wamezikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika sheria zangu.


kwa kuwa hukumtumikia BWANA, Mungu wako, kwa furaha na moyo wa kushukuru, kwa ajili ya ule wingi wa vitu vyote;


kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta BWANA juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.


Tena itakuwa, wakiisha kujiliwa na mambo maovu mengi na mashaka, utashuhudia wimbo huu mbele yao kama shahidi, kwa maana hautasahauliwa katika vinywa vya uzao wao; kwani nayajua mawazo yao wayawazayo, hata sasa kabla sijawatia katika nchi niliyoapa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo