Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nehemia 9:33 - Swahili Revised Union Version

33 Lakini wewe u mwenye haki, katika hayo yote yaliyotupata; maana wewe umetenda yaliyo kweli, lakini sisi tumetenda yaliyo maovu;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

33 Hata hivyo, unayo haki kwa kutuadhibu hivyo; kwani wewe umekuwa mwaminifu ambapo sisi tumekuwa watenda maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

33 Hata hivyo, unayo haki kwa kutuadhibu hivyo; kwani wewe umekuwa mwaminifu ambapo sisi tumekuwa watenda maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

33 Hata hivyo, unayo haki kwa kutuadhibu hivyo; kwani wewe umekuwa mwaminifu ambapo sisi tumekuwa watenda maovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

33 Lakini wewe u mwenye haki, katika hayo yote yaliyotupata; maana wewe umetenda yaliyo kweli, lakini sisi tumetenda yaliyo maovu;

Tazama sura Nakili




Nehemia 9:33
16 Marejeleo ya Msalaba  

La hasha! Usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha! Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?


Ee BWANA, Mungu wa Israeli, wewe ndiwe mwenye haki, maana sisi tumesalia, mabaki yaliyookoka, kama hivi leo; tazama, sisi tupo hapa wenye hatia mbele zako; maana hapana mtu awezaye kusimama mbele zako kwa sababu ya jambo hili.


na wafalme wetu, na wakuu wetu, na makuhani wetu, na baba zetu, hawakuishika sheria yako, wala hawakuzisikiliza amri zako na shuhuda zako, ulizowashuhudia.


nawe ukauona moyo wake kuwa mwaminifu mbele zako, ukafanya agano naye, kumpa nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Myebusi, na Mgirgashi, naam, kuwapa wazao wake; nawe umetimiza ahadi yako kwani u mwenye haki.


Yeye huimba mbele ya watu, na kusema, Mimi nimefanya dhambi, na kuyapotosha hayo yaliyoelekea, Wala sikulipizwa jambo hilo;


Kwani yeye hana haja ya kumfikiria mtu zaidi, ili aende mbele za Mungu ahukumiwe.


Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, Tumetenda maovu, tumefanya ubaya.


Ee BWANA, Wewe ndiwe mwenye haki, Na hukumu zako ni za adili.


BWANA ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye huruma katika matendo yake yote.


Musa akarejea kwa BWANA akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.


Wewe u mwenye haki, Ee BWANA, nitetapo nawe, lakini nitasema nawe katika habari ya haki. Mbona njia ya wabaya inasitawi? Mbona wote watendao hila wanakaa salama?


kwa sababu ya uovu wao, waliotenda ili kunikasirisha, kwa kuwa walikwenda kufukiza uvumba, na kuwatumikia miungu mingine, ambao hawakuwajua, wao, wala ninyi, wala baba zenu.


BWANA ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.


nanyi mtajua ya kuwa mimi ni BWANA; kwa maana hamuendi katika amri zangu, wala hamkuzishika hukumu zangu, bali mmetenda mambo kama hukumu za mataifa wanaowazunguka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo