Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nahumu 2:4 - Swahili Revised Union Version

4 Magari ya vita yanafanya vishindo njiani, Yanasonganasongana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Magari ya farasi yanatimua mbio barabarani, yanakwenda huko na huko uwanjani. Yanamulika kama miali ya moto! Yanakwenda kasi kama umeme.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Magari ya farasi yanatimua mbio barabarani, yanakwenda huko na huko uwanjani. Yanamulika kama miali ya moto! Yanakwenda kasi kama umeme.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Magari ya farasi yanatimua mbio barabarani, yanakwenda huko na huko uwanjani. Yanamulika kama miali ya moto! Yanakwenda kasi kama umeme.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani, yakikimbia nyuma na mbele uwanjani. Yanaonekana kama mienge ya moto; yanaenda kasi kama umeme.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Magari ya vita yanafanya msukosuko barabarani, yakikimbia nyuma na mbele uwanjani. Yanaonekana kama mienge ya moto; yanakwenda kasi kama umeme.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Magari ya vita yanafanya vishindo njiani, Yanasonganasongana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme.

Tazama sura Nakili




Nahumu 2:4
10 Marejeleo ya Msalaba  

Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.


Umemshutumu Bwana kwa watumishi wako, kwa kuwa umesema, Kwa wingi wa magari yangu nimepanda juu ya vilele vya milima, mpaka mahali pa ndani ya Lebanoni; nami nitaikata mierezi yake mirefu, na misonobari yake mizuri, nami nitaingia ndani ya mahali pake palipoinuka, palipo mbali sana, msitu wa shamba lake lizaalo sana.


Maana BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.


Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi wake ni wepesi kuliko tai. Ole wetu, kwa sababu tumeharibika.


Haya! Pandeni, enyi farasi; Jihimizeni, enyi magari ya vita; Mashujaa nao na watoke nje Kushi na Puti, watumiao ngao; Nao Waludi, washikao uta na kuupinda.


Nao watakuja kwako na silaha zao, na magari ya vita, na magurudumu, na wingi wa mataifa; watajipanga juu yako kwa ngao, na vigao, na chapeo za shaba, pande zote; nami nitawapa uwezo wa kuhukumu, nao watakuhukumu kulingana na hukumu zao.


Kwa sababu wingi wa farasi wake, mavumbi yao yatakufunika; kuta zako zitatetemeka kwa sababu ya mshindo wa wapanda farasi, na wa magurudumu, na wa magari ya vita, atakapoingia katika malango yako, kama watu waingiavyo katika mji uliobomolewa mahali.


Maana Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitamleta Nebukadneza, mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, juu ya Tiro toka kaskazini, pamoja na farasi, na magari ya vita, na wapanda farasi, na jeshi, na watu wengi.


Na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo