Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mwanzo 24:1 - Swahili Revised Union Version

1 Basi Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na BWANA alikuwa amembariki Abrahamu katika vitu vyote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Sasa Abrahamu alikuwa mzee wa miaka mingi, naye Mwenyezi-Mungu alikuwa amembariki katika kila hali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Sasa Abrahamu alikuwa mzee wa miaka mingi, naye Mwenyezi-Mungu alikuwa amembariki katika kila hali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Sasa Abrahamu alikuwa mzee wa miaka mingi, naye Mwenyezi-Mungu alikuwa amembariki katika kila hali.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Wakati huu Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Mwenyezi Mungu alikuwa amembariki katika mambo yote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Wakati huu Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye bwana alikuwa amembariki katika kila njia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Basi Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na BWANA alikuwa amembariki Abrahamu katika vitu vyote.

Tazama sura Nakili




Mwanzo 24:1
17 Marejeleo ya Msalaba  

nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;


Naye Abramu alikuwa tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha, na kwa dhahabu.


Basi Abrahamu na Sara walikuwa wazee wenye umri mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.


Naye Abrahamu alikuwa mtu wa miaka mia moja, alipozaliwa mwana wake Isaka.


na BWANA amembarikia sana bwana wangu, amekuwa mtu mkuu; amempa kondoo, na ng'ombe, na fedha, na dhahabu, na watumishi, na wajakazi, na ngamia, na punda.


Isaka akawa mwenye miaka arubaini alipomtwaa Rebeka binti Bethueli, Mshami, wa Padan-aramu, ndugu wa Labani, Mshami, kuwa mke wake.


Mwaka huo Isaka akapanda mbegu katika nchi ile, naye akapata mavuno mara mia zaidi. BWANA akambariki.


Naam, kwa Mungu wa baba yako atakayekusaidia; Kwa baraka za juu mbinguni. Baraka za vilindi vilivyo chini, Baraka za maziwa, na za mimba.


Mfalme Daudi alikuwa mzee, mkongwe katika siku zake, nao wakamfunika nguo, lakini asipate joto.


Baraka ya BWANA hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo.


Mwangalieni Abrahamu, baba yenu, na Sara, aliyewazaa; kwa maana alipokuwa mmoja tu nilimwita, nikambariki, nikamfanya kuwa wengi.


Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.


Nao walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili ni wazee sana.


Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Abrahamu aliyekuwa mwenye imani.


Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;


Maana, mazoezi ya viungo vya mwili yana manufaa kidogo, lakini utauwa una manufaa ya kila aina; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo