Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mika 7:13 - Swahili Revised Union Version

13 Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa, kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa, kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa, kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

13 Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.

Tazama sura Nakili




Mika 7:13
22 Marejeleo ya Msalaba  

Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.


Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.


Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.


Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, Naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.


Katika siku hiyo miji yake yenye maboma itakuwa kama mahali palipoachwa ndani ya mwitu, na juu ya kilele cha mlima, palipoachwa mbele ya wana wa Israeli; napo patakuwa ganjo.


Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.


Nami nitawaadhibu kwa kadiri ya matendo yenu, asema BWANA; nami nitawasha moto katika msitu wake, nao utateketeza vitu vyote viuzungukavyo.


Na nchi hii yote pia itakuwa ukiwa, na kitu cha kushangaza; nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli miaka sabini.


mkuu wa mashauri, muweza katika kutenda; ambaye macho yake yamefumbuka juu ya njia zote za wanadamu, kumpa kila mtu kwa kadiri ya njia zake, na kwa kadiri ya matunda ya matendo yake,


ukawaambie watu wa nchi, Bwana MUNGU asema hivi, kuhusu habari zao wakaao Yerusalemu, na katika nchi ya Israeli; Watakula chakula chao kwa kukitunza sana, na maji yao watayanywa kwa ushangao, nchi yao iwe ukiwa, kwa kukosa vitu vyote viijazavyo, kwa sababu ya udhalimu wao wote wakaao ndani yake.


Nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa na ajabu, na kiburi cha uwezo wake kitakoma; nayo milima ya Israeli itakuwa ukiwa, asipite mtu.


Basi, kwa ajili yenu, Sayuni utalimwa kama shamba lilimwavyo, na Yerusalemu utakuwa magofu; na mlima wa nyumba utakuwa kama mahali palipoinuka msituni.


Ndipo watakapomwomba BWANA, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.


Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na uchungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli.


Basi, kwa ajili ya hayo, mimi nami nimekupiga kwa pigo liumizalo sana; nimekufanya kuwa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo