Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mika 7:12 - Swahili Revised Union Version

12 Siku hiyo watakujia kutoka Ashuru na miji ya Misri, na kutoka Misri mpaka huo Mto, na kutoka bahari hii mpaka bahari hii, na kutoka mlima huu mpaka mlima huu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Siku hiyo ndugu zenu watawarudia, kutoka Ashuru na vijiji vya Misri, kutoka nchi ya Misri na eneo la Eufrate; kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Siku hiyo ndugu zenu watawarudia, kutoka Ashuru na vijiji vya Misri, kutoka nchi ya Misri na eneo la Eufrate; kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Siku hiyo ndugu zenu watawarudia, kutoka Ashuru na vijiji vya Misri, kutoka nchi ya Misri na eneo la Eufrate; kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Mto Frati, na kutoka bahari hadi bahari, na kutoka mlima hadi mlima.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

12 Siku hiyo watakujia kutoka Ashuru na miji ya Misri, na kutoka Misri mpaka huo Mto, na kutoka bahari hii mpaka bahari hii, na kutoka mlima huu mpaka mlima huu.

Tazama sura Nakili




Mika 7:12
15 Marejeleo ya Msalaba  

Na itakuwa katika siku hiyo, Bwana atapeleka mkono wake mara ya pili, ili ajipatie watu wake watakaosalia, kutoka Ashuru, na kutoka Misri, na kutoka Pathrosi, na kutoka Kushi, na kutoka Elamu, na kutoka Shinari, na kutoka Hamathi, na kutoka visiwa vya bahari.


Itakuwako njia kuu kwa mabaki ya watu wake watakaobaki, watokao Ashuru, kama vile ilivyokuwako kwa Israeli, katika siku ile waliyotoka katika nchi ya Misri.


nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia.


Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu.


Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka.


Siku zile nyumba ya Yuda watakwenda pamoja na nyumba ya Israeli, nao watakuja pamoja, kutoka nchi ya kaskazini, mpaka nchi ile niliyowapa baba zenu iwe urithi wao.


Tazama, nitawaleta toka nchi ya kaskazini, na kuwakusanya katika miisho ya dunia, na pamoja nao watakuja walio vipofu, na hao wachechemeao, mwanamke mwenye mimba, na yeye pia aliye na uchungu wa kuzaa; watarudi huko, jeshi kubwa.


Lakini usiogope wewe, Ee Yakobo, mtumishi wangu; wala usifadhaike, Ee Israeli; kwa maana, tazama, nitakuokoa toka mbali, na wazao wako toka nchi ya uhamisho wao; na Yakobo atarudi, naye atatulia na kustarehe, wala hapana mtu atakayemtia hofu.


Siku ile nitawachipushia nyumba ya Israeli pembe, nami nitakujalia kufumbua kinywa kati yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA.


Ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe;


Watakuja wakitetemeka kama shomoro, toka Misri, na kama hua, toka nchi ya Ashuru; nami nitawakalisha katika nyumba zao, asema BWANA.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo