Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mhubiri 1:8 - Swahili Revised Union Version

8 Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Mambo yote husababisha uchovu, uchovu mkubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Mambo yote husababisha uchovu, uchovu mkubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Mambo yote husababisha uchovu, uchovu mkubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Vitu vyote vinachosha, kuliko mtu anavyoweza kusema. Jicho kamwe halitosheki kutazama, wala sikio halishibi kusikia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Vitu vyote vinachosha, zaidi kuliko mtu anavyoweza kusema. Jicho kamwe halitosheki kutazama, wala sikio halishibi kusikia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

8 Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

Tazama sura Nakili




Mhubiri 1:8
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.


Kuzimu na Uharibifu havishibi; Wala macho ya wanadamu hayashibi.


Mito yote huingia baharini, lakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena.


Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kufukuza upepo, wala faida hakuna chini ya jua.


Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na kututa, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kufukuza upepo.


Kuna mtu aliye peke yake, wala hana mwenzi wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema? Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa.


Juhudi zote za binadamu ni kwa kinywa chake, Lakini hamu yake haitosheleki.


Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha mbali. Ni kwa sababu gani? Asema BWANA wa majeshi. Ni kwa sababu yumba yangu imebaki kuwa gofu la nyumba, wakati ambapo kila mmoja wenu anakimbilia nyumbani kwake.


Njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.


Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo