Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 8:13 - Swahili Revised Union Version

13 Kumcha BWANA ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu. Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya; nachukia na lugha mbaya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu. Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya; nachukia na lugha mbaya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu. Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya; nachukia na lugha mbaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Kumcha Mwenyezi Mungu ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Kumcha bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

13 Kumcha BWANA ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.

Tazama sura Nakili




Methali 8:13
27 Marejeleo ya Msalaba  

Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu.


Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.


Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.


Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.


Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Enyi mmpendao BWANA, uchukieni uovu; Huwalinda nafsi zao watauwa wake, Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.


Lakini hao wakunga walikuwa wacha Mungu, hawakufanya kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale watoto wa kiume.


Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima; Bali ulimi wa ukaidi utakatiliwa mbali.


Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.


Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.


Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA; Hakika, hatakosa adhabu.


Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.


Usiwe na hekima machoni pako; Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.


Jiepushe na kinywa cha ujeuri, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.


Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotovu.


Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayashusha chini majivuno yao walio wakali;


Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba BWANA, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.


Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema BWANA, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.


wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema BWANA.


Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkilishika lililo jema.


jitengeni na ubaya wa kila namna.


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa, Naye huyapima matendo kwa mizani.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo