Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 5:12 - Swahili Revised Union Version

12 Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu, na kudharau maonyo moyoni mwangu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu, na kudharau maonyo moyoni mwangu!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu, na kudharau maonyo moyoni mwangu!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

12 Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;

Tazama sura Nakili




Methali 5:12
23 Marejeleo ya Msalaba  

Wakasema, “Ondoka hapa!” Kisha wakasema, “Mtu huyu amekuja kukaa kwetu kama mgeni; naye kumbe anataka kuhukumu! Basi tutakutenda vibaya kuliko hawa”. Wakamsonga sana Lutu, wakakaribia wauvunje mlango.


Ikawa, aliposema naye, mfalme akamwambia, Je! Tumekutia wewe kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza; kwa nini upigwe? Ndipo yule nabii akaacha, akasema, Najua ya kuwa Mungu amekusudia kukuangamiza, kwa sababu umeyafanya haya, wala hukulisikiliza shauri langu.


lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.


Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.


Nilikuwa kama mjinga, sijui neno; Nilikuwa kama mnyama tu mbele zako.


Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga? Na wenye dharau kupenda dharau yao, Na wapumbavu kuchukia maarifa?


Bali mmeupuuza ushauri wangu, Wala hamkutaka maonyo yangu;


Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.


Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima; Bali yeye aachaye maonyo hukosa.


Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.


Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.


Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.


Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho, Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;


Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.


Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.


Tena nilituma kwenu watumishi wangu wote, manabii, nikiamka mapema na kuwatuma, nikisema, Basi ninyi; msilifanye chukizo hili linalochukiza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo