Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 30:10 - Swahili Revised Union Version

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake; Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake, asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake, asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake, asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 “Usimchongee mtumishi kwa bwana wake, asije akakulaani, ukapatilizwa kwalo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 “Usimchongee mtumishi kwa bwana wake, asije akakulaani, ukapatilizwa kwalo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake; Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

Tazama sura Nakili




Methali 30:10
18 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akasikia harufu ya kumridhisha; BWANA akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, maana mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya. 1


Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani; Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.


Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.


Tena, usitie moyoni mwako maneno yote wasemayo watu; usije ukamsikia mtumishi wako mwenyewe akikutukana.


Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danieli, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.


Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danieli, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu.


Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.


Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako.


Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako;


Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru?


Basi sasa, nakusihi, bwana wangu, mfalme, na asikie maneno ya mtumishi wake. Ikiwa ni BWANA aliyekuchochea juu yangu, na akubali sadaka; bali ikiwa ni wanadamu, na walaaniwe mbele za BWANA; kwa sababu wamenifukuza leo, nisishikamane na urithi wa BWANA, wakisema, Nenda, ukatumikie miungu mingine.


Daudi akamwambia, Je! Wewe utaniongoza chini hadi nilifikie jeshi hilo? Naye akasema, Uniapie kwa Mungu, ya kwamba hutaniua, wala kunitia mikononi mwa huyo bwana wangu, nami nitakuongoza chini hata kulifikia jeshi hilo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo