Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 29:4 - Swahili Revised Union Version

4 Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti, lakini akipenda hongo taifa huangamia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti, lakini akipenda hongo taifa huangamia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti, lakini akipenda hongo taifa huangamia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Tazama sura Nakili




Methali 29:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Daudi akatawala juu ya Israeli wote; naye Daudi akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.


Basi Sulemani akaketi katika kiti cha enzi cha Daudi baba yake; na ufalme wake ukawa imara sana.


Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti chake cha enzi, kuwa mfalme wake BWANA, Mungu wako; kwa kuwa Mungu wako amewapenda Israeli, kuwathibitisha milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme juu yao, ufanye hukumu na haki.


Tena akuoneshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.


Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zimo mbele za uso wako.


Mfalme mkuu upendaye hukumu kwa haki; Umeiimarisha haki; Umefanya hukumu na haki katika Israeli.


Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wowote.


Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme; Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.


Wafalme wakitenda yasiyo haki ni chukizo; Maana kiti cha enzi huthibitika kwa haki.


Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.


Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.


Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.


BWANA asema hivi, Wakati uliokubalika nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa;


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Ndipo badala yake atasimama mmoja, atakayepitisha mwenye kutoza ushuru kati ya utukufu wa ufalme wake; lakini katika muda wa siku chache ataangamizwa, si kwa hasira, wala si katika vita.


Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.


Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya BWANA, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana BWANA angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo