Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 28:15 - Swahili Revised Union Version

15 Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Mtawala mwovu anayewatawala maskini, ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Mtawala mwovu anayewatawala maskini, ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Mtawala mwovu anayewatawala maskini, ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu anayetawala wanyonge.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

15 Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

Tazama sura Nakili




Methali 28:15
19 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Menahemu akapiga Tifsa, na wote waliokuwamo, na mipaka yake, toka Tirza; kwa sababu hawakumfungulia, kwa hiyo akaupiga; nao wanawake wote waliokuwamo wenye mimba akawapasua.


Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la BWANA. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arubaini na wawili miongoni mwao.


Na Manase akazimwaga damu zisizo na hatia, nyingi sana, hata alipokuwa ameijaza Yerusalemu tangu upande huu hata upande huu; zaidi ya kosa lake alilowakosesha Yuda, kutenda yaliyo mabaya machoni pa BWANA.


Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali;


Kisha huyo Farao akawaagiza watu wake wote, akisema, Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa mtamtupa mtoni, na kila mtoto wa kike mtamhifadhi hai.


Afadhali mtu akutwe na dubu jike aliyenyang'anywa watoto wake, Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake.


Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; Bali hisani yake kama umande juu ya majani.


Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.


Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.


BWANA amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.


Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu.


nitawajia kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.


Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.


Wakuu wake walio ndani yake ni simba wangurumao; mahakimu wake ni mbwamwitu wa jioni; wasiobakiza kitu chochote mpaka asubuhi.


Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale majusi, alighadhibika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wa kiume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake kote, kuanzia wenye miaka miwili na chini yake, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale majusi.


Muwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo