Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 25:2 - Swahili Revised Union Version

2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo, lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo, lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo, lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.

Tazama sura Nakili




Methali 25:2
20 Marejeleo ya Msalaba  

Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Umejuaje ya kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?


Mfalme akasema, Je! Si mkono wa Yoabu ulio pamoja nawe katika haya yote? Mwanamke akajibu, akasema, Kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mfalme, hapana mtu awezaye kugeuka kwa kulia, au kwa kushoto, kukana neno lolote alilolisema bwana wangu mfalme; kwani mtumishi wako Yoabu ndiye aliyeniamuru, na kuyaweka maneno haya yote kinywani mwa mjakazi wako;


Ili habari zichunguzwe katika kitabu cha kumbukumbu za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha kumbukumbu ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na wakuu wa mikoa, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.


Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umewaasi wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.


Basi, sasa, mfalme akiona vema, watu na wachunguze katika nyumba ya hazina ya mfalme, iliyoko huko Babeli, kama ni kweli ya kuwa mfalme Koreshi alitoa amri kuijenga nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu, na mfalme akatutumie habari ya mapenzi yake kuhusu jambo hili.


Ndipo mfalme Dario akatoa amri, na watu wakachunguza katika nyumba ya kuhifadhia vitabu vya kumbukumbu ambapo hati ziliwekwa katika Babeli.


Nilikuwa baba kwa mhitaji, Na kesi ya mtu nisiyemjua niliichunguza.


Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama una ufahamu.


Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye.


Ni nani huyu afichaye ushauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.


Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.


Mbingu huenda juu sana, na nchi huenda chini; Lakini mioyo ya wafalme haichunguziki.


Nikatia moyo wangu ili kuyatafuta yote yanayotendeka chini ya mbingu, na kuyavumbua kwa hekima; ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.


BWANA akawang'oa katika nchi yao kwa hasira, na ghadhabu, na makamio makuu, akawatupa waende nchi nyingine, kama hivi leo.


Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo