Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 16:24 - Swahili Revised Union Version

24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

24 Maneno mazuri ni kama asali; ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

24 Maneno mazuri ni kama asali; ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

24 Maneno mazuri ni kama asali; ni matamu rohoni na yenye kuupa mwili afya.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

24 Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali, ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

24 Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali, ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

Tazama sura Nakili




Methali 16:24
18 Marejeleo ya Msalaba  

Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu.


Ni za kutamanika kuliko dhahabu, Kuliko wingi wa dhahabu safi. Nazo ni tamu kuliko asali, Kuliko sega la asali.


Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.


Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!


Ushauri mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali maneno yapendezayo ni safi.


Moyo uliochangamka ni dawa nzuri; Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.


Naam, viuno vyangu vitafurahi, Midomo yako inenapo maneno mema.


Marhamu na manukato huufurahisha moyo; Kadhalika utamu wa rafiki ya mtu utokao katika kusudi la moyo wake.


Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako.


Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote.


Huyo Mhubiri akachunguza ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.


Bibi arusi, midomo yako yadondosha asali, Asali na maziwa viko chini ya ulimi wako; Na harufu ya mavazi yako Ni kama harufu ya Lebanoni.


Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA, Mungu wa majeshi.


Mafundisho yangu yatadondoka kama mvua, Maneno yangu yatatona-tona kama umande; Kama manyunyu juu ya majani mabichi; Kama matone ya mvua juu ya mimea.


Nikakitwaa kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa malaika yule, nikakila; nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu, na nilipokwisha kukila tumbo langu likatiwa uchungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo