Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Matendo 16:5 - Swahili Revised Union Version

5 Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Hivyo makundi ya waumini yakaimarika katika imani, na wakaongezeka kwa idadi kila siku.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Hivyo makundi ya waumini yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.

Tazama sura Nakili




Matendo 16:5
23 Marejeleo ya Msalaba  

Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwaminini BWANA, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa.


tena kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia. Ikiwa hamtasimama imara katika imani, hamtathibitika kamwe.


Mkono wa Bwana ukawa pamoja nao, watu wengi wakaamini, wakamwelekea Bwana.


Neno la Bwana likazidi na kuenea.


Akapita katika Shamu na Kilikia akiyaimarisha makanisa.


wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.


Lakini wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya wanaume ikawa kama elfu tano.


walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake;


Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.


Basi kanisa likapata raha kote katika Yudea na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.


Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na Injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele,


Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mnajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.


Katika uhuru huo Kristo alituweka huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.


Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, ishini vivyo hivyo katika yeye;


apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.


Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji katika imani yenu;


Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,


Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.


Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawaimarisha, atawathibitisha, atawatia nguvu na kuwapa msingi imara.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo