Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Maombolezo 3:37 - Swahili Revised Union Version

37 Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

37 Nani awezaye kuamuru kitu kifanyike Mwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

37 Nani awezaye kuamuru kitu kifanyike Mwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

37 Nani awezaye kuamuru kitu kifanyike Mwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

37 Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

37 Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

37 Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?

Tazama sura Nakili




Maombolezo 3:37
16 Marejeleo ya Msalaba  

Mfalme akasema, Nina nini na ninyi, enyi wana wa Seruya? Kwa sababu yeye analaani, na kwa sababu BWANA amemwambia, Mlaani Daudi, basi, ni nani atakayesema, Mbona umetenda haya?


Mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari lake, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.


Hata alipokuwa katika kusema nao, tazama, yule aliyetumwa akamshukia; naye akasema, Angalia, mabaya haya yatoka kwa BWANA; kwani mimi kumngojea BWANA tena?


Lakini mambo haya uliyaficha moyoni mwako; Najua kuwa haya yamo nafsini mwako;


Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.


Lakini akawaambia, Ehe, BWANA na awe pamoja nanyi, kama nitakavyowapa ruhusa kwenda zenu pamoja na watoto wenu; angalieni, kwa kuwa pana uovu huko mbele yenu.


Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali BWANA huziongoza hatua zake.


Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la BWANA ndilo litakalosimama.


Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya BWANA.


nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.


Tazama, mimi niko juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA.


na watu wote wanaokaa duniani wamehesabiwa kuwa si kitu, naye hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, Unafanya nini wewe?


Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.


na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo