Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Luka 6:30 - Swahili Revised Union Version

30 Mpe kila akuombaye, na akunyang'anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyanganya mali yako usimtake akurudishie.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyanganya mali yako usimtake akurudishie.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

30 Mpe kila akuombaye, na akunyang'anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.

Tazama sura Nakili




Luka 6:30
29 Marejeleo ya Msalaba  

Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.


Heri amkumbukaye mnyonge; BWANA atamwokoa siku ya taabu.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa; Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.


Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.


Uwagawie sehemu watu saba, hata wanane; Maana hujui baa gani litakalokuwa juu ya nchi.


Mimi nilipotia moyo wangu katika kuijua hekima, na kuuona utumishi uliofanyika juu ya nchi, (maana kuna asiyepata usingizi kwa macho yake mchana wala usiku);


Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.


Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kulia, mgeuzie na la pili.


Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.


Lakini, toeni sadaka vile vya ndani, na tazama, vyote huwa safi kwenu.


Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, akiba isiyopungua katika mbingu, mahali pasipokaribia mwizi, wala nondo haharibu.


Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.


Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang'anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.


Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo.


Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.


Mwizi asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akifanya kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo