Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 42:21 - Swahili Revised Union Version

21 BWANA akapendezwa, kwa ajili ya haki yake, kuitukuza sheria, na kuiadhimisha.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

21 Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya uaminifu wake, alipenda kukuza mwongozo wake na kuutukuza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

21 Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya uaminifu wake, alipenda kukuza mwongozo wake na kuutukuza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

21 Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya uaminifu wake, alipenda kukuza mwongozo wake na kuutukuza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

21 Ilimpendeza Mwenyezi Mungu kwa ajili ya haki yake kufanya sheria yake kuwa kuu na tukufu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

21 Ilimpendeza bwana kwa ajili ya haki yake kufanya sheria yake kuwa kuu na tukufu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

21 BWANA akapendezwa, kwa ajili ya haki yake, kuitukuza sheria, na kuiadhimisha.

Tazama sura Nakili




Isaya 42:21
32 Marejeleo ya Msalaba  

Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, Nitalishukuru jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, Kwa maana umeikuza ahadi yako, na jina lako juu ya vyote.


Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.


Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako.


Na haki yako, Ee Mungu, Imefika juu sana. Wewe uliyefanya mambo makuu; Ee Mungu, ni nani aliye kama Wewe?


Hatazimia, wala hatakata tamaa, hata atakapoweka hukumu duniani; na visiwa vitaingojea sheria yake.


Nisikilizeni mimi, enyi watu wangu; nisikieni, taifa langu; maana sheria itatoka kwangu, na kutoa haki yangu iwe nuru ya mataifa.


Alipokuwa bado akisema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.


Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Ndipo akakubali.


na tazama, sauti kutoka mbinguni ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.


Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.


Naye aliyenituma yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.


Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.


Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? La hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.


Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.


Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;


Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, hakika haki ingalipatikana kwa sheria.


Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili.


Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo?


tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani;


Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika fikira zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo