Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 27:8 - Swahili Revised Union Version

8 Umemwadhibu kwa kiasi, ulipomfukuza; ukampepeta kwa upepo mkali katika siku ya upepo wa mashariki.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni. Wakati wa upepo mkali wa mashariki, aliwaondoa kwa kipigo kikali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni. Wakati wa upepo mkali wa mashariki, aliwaondoa kwa kipigo kikali.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni. Wakati wa upepo mkali wa mashariki, aliwaondoa kwa kipigo kikali.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

8 Umemwadhibu kwa kiasi, ulipomfukuza; ukampepeta kwa upepo mkali katika siku ya upepo wa mashariki.

Tazama sura Nakili




Isaya 27:8
33 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza.


Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.


Yeye hatashutumu daima, Wala hatashika hasira yake milele.


Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako, Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.


BWANA, usinikemee kwa hasira yako, Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.


Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.


Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.


Mbona mnataka kupigwa, hata sasa, hata mkazidi kuasi? Kichwa chote ni kigonjwa, moyo wote umezimia.


Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitamwadhibu matunda ya kiburi cha moyo wake mfalme wa Ashuru, na majivuno ya macho yake.


BWANA asema hivi, Iko wapi hati ya talaka ya mama yenu, ambayo kwa hiyo niliachana naye? Au nimewauza ninyi kwa nani katika watu wanaoniwia? Ninyi mliuzwa kwa sababu ya maovu yenu; tena mama yenu ameachwa kwa sababu ya makosa yenu.


Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakurudisha.


Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya.


Wewe wamlaki yeye afurahiaye yaliyo haki na kuyatenda, watu wale wakukumbukao katika njia zako; tazama, ulikuwa na hasira, nasi tulitenda dhambi; tumekuwa katika dhambi kwa muda mrefu, nasi Je! Tutaokolewa?


Ee BWANA, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza.


Maana mimi ni pamoja nawe, asema BWANA, nikuokoe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokutawanya, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu.


Wakati ule watu hawa na Yerusalemu wataambiwa neno hili, Upepo wa moto utokao katika vilele vya nyikani visivyo na miti, ukimwelekea binti ya watu wangu, hauwi upepo wa kupepeta, wala upepo wa kutakasa;


Maana BWANA asema hivi, Nchi yote itakuwa ukiwa; lakini sitaikomesha kabisa.


Usiogope wewe, Ee Yakobo, mtumishi wangu, asema BWANA; kwa maana mimi ni pamoja nawe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokufukuza, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu.


Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.


Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.


Lakini aling'olewa kwa ghadhabu, akaangushwa chini, upepo wa mashariki ukakausha matunda yake; vijiti vyake vya nguvu vikavunjika, vikakauka; moto ulivila.


Ajapokuwa yeye ni mwenye kuzaa sana kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja, hiyo pumzi ya BWANA itokayo upande wa nyikani, na kijito chake cha maji kitakauka, na chemchemi yake itakaushwa; yeye atateka nyara hazina ya vyombo vyote vipendezavyo.


Lisikieni neno la BWANA, enyi wana wa Israeli; kwa maana BWANA ana shutuma nao wakaao katika nchi, kwa sababu hapana kweli, wala fadhili, wala kumjua Mungu katika nchi.


Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili muweze kustahimili.


Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa muda mfupi, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo