Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 25:3 - Swahili Revised Union Version

3 Kwa hiyo watu walio hodari watakutukuza, Miji ya mataifa yatishayo itakuogopa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa katili itakuogopa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa katili itakuogopa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa katili itakuogopa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuogopa wewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Kwa hiyo watu walio hodari watakutukuza, Miji ya mataifa yatishayo itakuogopa.

Tazama sura Nakili




Isaya 25:3
16 Marejeleo ya Msalaba  

Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako, Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako.


Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayashusha chini majivuno yao walio wakali;


Basi, mtukuzeni BWANA katika mashariki, litukuzeni jina la BWANA, Mungu wa Israeli, katika visiwa vya bahari.


Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi laini, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafla.


Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA.


Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa BWANA, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako.


Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, BWANA wa majeshi, na kuiadhimisha sikukuu ya Vibanda.


Naye BWANA atakuwa Mfalme wa nchi yote; siku hiyo BWANA atakuwa mmoja, na jina lake moja.


Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliobakia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo