Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 17:4 - Swahili Revised Union Version

4 Tena itakuwa katika siku hiyo, utukufu wa Yakobo utapungua na kunona kwa mwili wake kutakwisha.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 “Siku hiyo, fahari ya Yakobo itaporomoshwa, na unono wake ataupoteza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 “Siku hiyo, fahari ya Yakobo itaporomoshwa, na unono wake ataupoteza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 “Siku hiyo, fahari ya Yakobo itaporomoshwa, na unono wake ataupoteza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 Tena itakuwa katika siku hiyo, utukufu wa Yakobo utapungua na kunona kwa mwili wake kutakwisha.

Tazama sura Nakili




Isaya 17:4
15 Marejeleo ya Msalaba  

Na tazama, ng'ombe saba wengine wakapanda nyuma yao kutoka mtoni, wabaya, wamekonda, wakasimama karibu na wale ng'ombe wengine ukingoni mwa mto.


Naye Shalmanesa mfalme wa Ashuru akakwea juu yake, Hoshea akawa mtumishi wake, akampa kodi.


Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, huyo mfalme wa Ashuru akautwaa Samaria, akawahamisha Israeli mpaka Ashuru, akawaweka katika Hala na Habori, karibu na mto wa Gozani, na katika miji ya Wamedi.


Kwa hiyo Bwana, BWANA wa majeshi, atatuma maradhi ya kukondesha kwa wapiganaji walionenepa; na badala ya utukufu wake kutawashwa kuteketea kama kuteketea kwa moto.


Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! Mtamkimbilia nani mpate msaada? Na utukufu wenu mtauacha wapi?


Watainama chini ya wafungwa tu, wataanguka chini yao waliouawa. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


Na ngome ya Efraimu itakomeshwa, na ufalme wa Dameski, na mabaki ya Shamu; watakuwa kama utukufu wa wana wa Israeli, asema BWANA wa majeshi.


Maana katikati ya dunia, katikati ya mataifa, itakuwa hivi; kama wakati utikiswapo mzeituni, kama wakati waokotapo zabibu baada ya mavuno yake.


Toka pande za mwisho wa dunia tumesikia nyimbo, Atukuzwe mwenye haki. Ndipo niliposema, Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu! Watenda hila wametenda hila, naam, watendao hila wametenda hila sana.


Manase anamla Efraimu, naye Efraimu anamla Manase; nao wawili pamoja watakuwa juu ya Yuda. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.


Bwana alimpelekea Yakobo neno, nalo likamfikia Israeli.


Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU awaambia hivi; Tazama, mimi, naam, mimi, nitahukumu kati ya wanyama walionona na wanyama waliokonda.


Haya ndiyo asemayo BWANA; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao Samaria katika pembe ya kochi, na juu ya mito ya hariri ya kitanda.


BWANA atakuwa wa kutisha sana kwao; kwa maana atawaua kwa njaa miungu yote ya dunia; na watu watamsujudia yeye, kila mtu toka mahali pake; naam, nchi zote za mataifa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo