Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 15:1 - Swahili Revised Union Version

1 Ufunuo juu ya Moabu. Maana katika usiku mmoja Ari wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa; maana katika usiku mmoja Kiri wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Kauli ya Mungu dhidi ya nchi ya Moabu. Mji wa Ari nchini Moabu umeangamizwa usiku; mji wa Kiri nchini Moabu umeteketezwa usiku.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Kauli ya Mungu dhidi ya nchi ya Moabu. Mji wa Ari nchini Moabu umeangamizwa usiku; mji wa Kiri nchini Moabu umeteketezwa usiku.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Kauli ya Mungu dhidi ya nchi ya Moabu. Mji wa Ari nchini Moabu umeangamizwa usiku; mji wa Kiri nchini Moabu umeteketezwa usiku.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Neno la unabii kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Ufunuo juu ya Moabu. Maana katika usiku mmoja Ari wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa; maana katika usiku mmoja Kiri wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa.

Tazama sura Nakili




Isaya 15:1
20 Marejeleo ya Msalaba  

Wakaibomoa ile miji; wakatupa katika kila mahali palipo pema kila mtu jiwe lake, wakapajaza; wakaziziba chemchemi zote za maji, wakaikata miti yote iliyo mizuri; mpaka katika Kir-haresethi tu wakayasaza mawe yake; ila wenye kombeo wakauzunguka wakaupiga.


Nao watashuka, watalirukia bega la Wafilisti upande wa magharibi; nao pamoja watawateka wana wa mashariki; watanyosha mkono juu ya Edomu na Moabu; na wana wa Amoni watawatii.


Ufunuo juu ya Babeli; maono aliyoyaona Isaya, mwana wa Amozi.


Ufunuo huu ulikuja mwaka ule alipokufa mfalme Ahazi.


Kwa sababu hiyo mtima wangu unamlilia Moabu kama kinubi, na nafsi yangu kwa ajili ya Kir-Heresi.


Tumesikia habari za kiburi cha Moabu, ya kwamba ni mwenye kiburi kingi; habari za majivuno yake, na kiburi chake, na ghadhabu yake; majivuno yake si kitu.


Kwa sababu hiyo Moabu atalia kwa ajili ya Moabu, kila mmoja atalia, maana mtaiombolezea mikate ya zabibu ya Kir-Haresethi, mkipigwa sana.


Kwa maana mkono wa BWANA utatulia katika mlima huu, na Moabu atakanyagwa chini huko aliko, kama vile majani makavu yakanyagwavyo katika maji machafu.


Na boma la ngome ya kuta zako ameliinamisha, na kulilaza chini, na kulitupa chini hadi mavumbini.


Misri, na Yuda, na Edomu, na wana wa Amoni, na Moabu, na wote wenye kunyoa denge, wakaao nyikani; maana mataifa hayo yote hawana tohara, wala nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa mioyo yao.


Maana, moto umetoka Heshboni, Umekuwa Ari ya Moabu, Mwali wa moto umetoka mji wa Sihoni; Wakuu wa mahali palipoinuka Arnoni.


Hivi leo ivuke Ari, mpaka wa Moabu;


na utakaposongea kuwaelekea wana wa Amoni, usiwasumbue wana wa Amoni, wala usishindane nao; kwa kuwa sitakupa katika nchi ya hao wana wa Amoni kuwa milki yako; kwa sababu nimewapa wana wa Lutu iwe milki yao.


BWANA akaniambia, Usiwasumbue Wamoabi, wala usishindane nao katika mapigano; kwa kuwa sitakupa katika nchi yake kuimiliki; kwa sababu Ari nimewapa wana wa Lutu kuimiliki.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo