Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Hesabu 23:7 - Swahili Revised Union Version

7 Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo, Njoo! Unishutumie Israeli.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Balaamu akamtolea Balaki kauli yake, akasema, “Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, naam, mfalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki. ‘Njoo uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, naam, njoo uwalaumu Waisraeli!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Balaamu akamtolea Balaki kauli yake, akasema, “Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, naam, mfalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki. ‘Njoo uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, naam, njoo uwalaumu Waisraeli!’

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Balaamu akamtolea Balaki kauli yake, akasema, “Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, naam, mfalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki. ‘Njoo uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, naam, njoo uwalaumu Waisraeli!’

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Ndipo Balaamu akasema ujumbe wake: “Balaki amenileta kutoka Aramu, mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki. Akasema, ‘Njoo, unilaanie Yakobo; njoo unishutumie Israeli.’

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Ndipo Balaamu akasema ujumbe wake: “Balaki amenileta kutoka Aramu, mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki. Akasema, ‘Njoo, unilaanie Yakobo; njoo unishutumie Israeli.’

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo, Njoo! Unishutumie Israeli.

Tazama sura Nakili




Hesabu 23:7
31 Marejeleo ya Msalaba  

Wana wa Shemu ni Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu.


Ondoka, uende Padan-aramu, mpaka nyumba ya Bethueli baba ya mama yako, ukajitwalie huko mke katika binti za Labani, ndugu wa mama yako.


na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu.


Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shimei, nduguye Daudi, akamwua.


Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;


Kisha Ayubu akaendelea na hoja yake, na kusema,


Kisha Ayubu akaendelea na hoja yake, na kusema,


Kwa nini niogope wakati wa shida, Ubaya ukinizunguka miguuni pangu?


Nitafumbua kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale.


Kama shomoro katika kutangatanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpati mtu.


Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli mithali;


Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, wao hunisema; Je! Mtu huyu si mtu mwenye kupiga mithali?


Siku hiyo watatunga mithali juu yenu, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni nyingi, na kusema, Sisi tumeangamizwa kabisa; Yeye analibadili fungu la watu wangu; Jinsi anavyoniondolea hilo! Awagawia waasi mashamba yetu.


Je! Hawa wote hawatapiga mfano juu yake, na mithali ya kusimanga juu yake, wakisema, Ole wake yeye aongezaye kisicho mali yake! Hata lini? Na ole wake yeye ajitwikaye mzigo wa rehani!


Tazama, kuna watu waliotoka Misri, wanaufunika uso wa nchi; basi njoo unilaanie watu hawa; labda nitaweza kupigana nao, na kuwafukuza.


maana nitakutunukia heshima kubwa sana, na neno lolote utakaloniomba nitalitenda; basi njoo, nakusihi, unilaanie watu hawa.


Naye akatunga mithali yake, akasema, Ondoka Balaki, ukasikilize; Nisikilize, Ee mwana wa Sipori;


Akarudi kwake, na tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, yeye na wakuu wote wa Moabu pamoja naye.


Akatunga mithali yake akasema, Balaamu mwana wa Beori asema, Yule mtu aliyefumbwa macho asema,


Kisha akamwangalia Mkeni, akatunga mithali yake, akasema, Makao yako yana nguvu, Na kiota chako kimewekwa katika jabali.


Akatunga mithali yake akasema, Ole wao! Ni nani atakayepona, Mungu atakapofanya haya?


Akatunga mithali yake, akasema, Balaamu mwana wa Beori asema, Yule mtu aliyefumbuliwa macho asema;


Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia.


ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu kuumbwa kwa ulimwengu.


Nao wakataka kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.


kwa sababu hapo mlipotoka Misri hawakuwalaki na chakula wala maji njiani; na kwa kuwa walimwajiri juu yako Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyo Mesopotamia, aje akuapize.


Yule Mfilisti akasema, Nayatukana leo majeshi ya Israeli; nipeni mtu tupigane.


Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.


Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo