Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Danieli 4:3 - Swahili Revised Union Version

3 Ishara zake ni kubwa kama nini! Na maajabu yake yana uweza kama nini! Ufalme wake ni ufalme wa milele; na mamlaka yake ni ya kizazi hata kizazi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Jinsi gani zilivyo kubwa ishara zake Mungu! Maajabu yake ni makuu mno! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake yadumu kizazi hata kizazi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Jinsi gani zilivyo kubwa ishara zake Mungu! Maajabu yake ni makuu mno! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake yadumu kizazi hata kizazi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Jinsi gani zilivyo kubwa ishara zake Mungu! Maajabu yake ni makuu mno! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake yadumu kizazi hata kizazi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Ishara zake ni kuu kama nini! Na maajabu yake yana nguvu kama nini! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kizazi hadi kizazi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.

Tazama sura Nakili

Swahili Roehl Bible 1937

3 Vistaajabuni vielekezo vyake vilivyo vikuu! Navyo vioja vyake vilivyo vya nguvu! Ufalme wake ni ufalme wa kale na kale, nayo enzi yake ni ya vizazi na vizazi.

Tazama sura Nakili




Danieli 4:3
29 Marejeleo ya Msalaba  

Enzi na hofu zi pamoja na Mungu; Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.


Ee BWANA, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Kwa hekima umevifanya vyote pia. Dunia imejaa viumbe wako.


Akatenda mambo ya ishara zake kati yao, Na miujiza katika nchi ya Hamu.


Ufalme wako ni ufalme wa milele, BWANA ni mwaminifu katika maneno yake yote, Na mwenye fadhili katika matendo yake yote Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.


Atawalaye kwa uweza wake milele; Ambaye macho yake yanaangalia mataifa; Hebu wanaoasi wasijitukuze nafsi zao.


Na ahimidiwe BWANA, Mungu, Mungu wa Israeli, Atendaye miujiza Yeye peke yake;


Njia yako ilikuwa katika bahari. Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; Hatua zako hazikujulikana.


Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako.


Ee BWANA, jinsi yalivyo makuu matendo yako! Mawazo yako ni mafumbo makubwa.


Ee BWANA, wewe u Mungu wangu; Nitakutukuza na kulihimidi jina lako; Kwa kuwa umetenda mambo ya ajabu, Mashauri ya kale, kwa uaminifu na kweli.


Hayo nayo yatoka kwa BWANA wa majeshi, mwenye shauri la ajabu, apitaye wote kwa hekima yake.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Bali BWANA ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.


Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na walozi, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.


Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.


Hukumu hii imekuja kwa agizo la walinzi, na amri hii kwa neno la watakatifu; kusudi walio hai wapate kujua ya kuwa Aliye Juu anatawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, tena humtawaza juu yake aliye mnyonge.


Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.


Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye Juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.


Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!


Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa kutoka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, ishara, maajabu, vita, mkono hodari, mkono ulionyoshwa, na vitisho vikuu, kama vile BWANA, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu?


Sasa kwa Mfalme wa milele, asiyeweza kuona uharibifu, asiyeonekana, Mungu peke yake, na iwe heshima na utukufu milele na milele. Amina.


Lakini kuhusu Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya haki.


Mungu naye akishuhudia pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa karama za Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe.


Mtu akisema, na aseme kama asemaye maneno halisi ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.


Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo