Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Amosi 8:5 - Swahili Revised Union Version

5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandaa ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Mnajisemea mioyoni mwenu: “Sikukuu ya mwezi mwandamo itakwisha lini ili tuanze tena kuuza nafaka yetu? Siku ya Sabato itakwisha lini ili tupate kuuza ngano yetu? Tutatumia vipimo hafifu vya wastani na uzito, tutadanganya watu kwa mizani isizo sawa,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Mnajisemea mioyoni mwenu: “Sikukuu ya mwezi mwandamo itakwisha lini ili tuanze tena kuuza nafaka yetu? Siku ya Sabato itakwisha lini ili tupate kuuza ngano yetu? Tutatumia vipimo hafifu vya wastani na uzito, tutadanganya watu kwa mizani isizo sawa,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Mnajisemea mioyoni mwenu: “Sikukuu ya mwezi mwandamo itakwisha lini ili tuanze tena kuuza nafaka yetu? Siku ya Sabato itakwisha lini ili tupate kuuza ngano yetu? Tutatumia vipimo hafifu vya wastani na uzito, tutadanganya watu kwa mizani isizo sawa,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandaa ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu;

Tazama sura Nakili




Amosi 8:5
24 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Kwa nini kumwendea leo? Sio mwandamo wa mwezi, wala sabato. Akasema, Si neno.


Kisha, nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati yenu na mimi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.


Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa BWANA; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.


Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA; Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.


Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA; Tena mizani ya hila si njema.


Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mwandamo na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.


Kama ukigeuza mguu wako usiivunje sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya BWANA yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe;


Ni mfanya biashara, aliye na mizani ya udanganyifu mkononi mwake; anapenda kudhulumu.


Naye Efraimu alisema, Kweli nimekuwa tajiri, nimejipatia mali nyingi; katika kazi zangu zote hawataona kwangu uovu wowote uliokuwa dhambi.


Mizani ya haki, vipimo vya haki, efa ya haki, hini ya haki, ndivyo mtakavyokuwa navyo. Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri.


Nikasema, Ni kitu gani? Akasema, Kitu hiki ni efa itokeayo. Tena akasema, Huu ndio uovu wao katika nchi hii yote;


Akasema, Huyu ni Uovu; akamsukuma ndani ya kile kikapu; akalitupa lile jiwe la risasi juu ya mdomo wa ile efa.


Tena mwasema, Tazama, jambo hili linatuchokesha namna gani! Nanyi mmelidharau, asema BWANA wa majeshi; nanyi mmeleta kitu kilichopatikana kwa udhalimu, na kilema, na kilicho kigonjwa; ndivyo mnavyoleta sadaka; je! Niikubali hii mikononi mwenu? Asema BWANA.


Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;


Naye Daudi akamwambia Yonathani, Tazama, kesho ni mwandamo wa mwezi, nami hainipasi kukosa kuketi chakulani pamoja na mfalme; lakini niache nijifiche bondeni hadi siku ya tatu jioni.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo