Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Timotheo 4:7 - Swahili Revised Union Version

7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;

Tazama sura Nakili




2 Timotheo 4:7
22 Marejeleo ya Msalaba  

Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.


tena tangu waliopata umri wa miaka hamsini wasiendelee kuhudumu tena;


Lakini yeye alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.


Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia.


Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.


Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenituma, nikaimalize kazi yake.


Naye Yohana alipokuwa akimaliza mwendo wake alinena, Mnadhani mimi ni nani? Mimi siye. Lakini, angalieni, anakuja mmoja nyuma yangu ambaye mimi sistahili kumlegezea viatu vya miguu yake.


Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Nami nilikwenda kwa kuwa nilifunuliwa, nikawaeleza Injili ile niihubiriyo katika Mataifa, lakini kwa faragha kwa hao viongozi waliosifika, isiwe labda napiga mbio bure, au nilipiga mbio bure.


mkiwa na mashindano yale yale mliyoyaona kwangu, na kusikia kwamba ninayo hata sasa.


Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyonenwa awali juu yako, ili katika hayo uweze kupigana vile vita vizuri;


Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi.


Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na mazungumzo yasiyo ya kimungu, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo;


Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu.


Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,


Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.


Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu.


Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wasubiri bado muda mchache, hadi itakapotimia idadi ya watumishi wenzao na ndugu zao, watakaouawa kama wao walivyouawa.


ili kwamba vizazi vya wana wa Israeli wapate kujua ili kuwafundisha vita, hasa wao ambao hawakujua vita kabla ya wakati ule;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo