Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Wafalme 20:7 - Swahili Revised Union Version

7 Ndipo mfalme wa Israeli, akawaita wazee wote wa nchi, akasema, Angalieni, nawaomba, mwone, kwamba huyu ataka madhara; maana ametuma kwangu kutaka wake zangu na watoto wangu; na fedha yangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Ndipo Ahabu mfalme wa Israeli, akawaita viongozi wote wa nchi, akawaambia, “Sasa, oneni jinsi jamaa huyu anavyotaka kututaabisha! Ametuma ujumbe kwamba anataka wake zangu, watoto wangu, dhahabu na fedha yangu. Nami sikumkatalia!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Ndipo Ahabu mfalme wa Israeli, akawaita viongozi wote wa nchi, akawaambia, “Sasa, oneni jinsi jamaa huyu anavyotaka kututaabisha! Ametuma ujumbe kwamba anataka wake zangu, watoto wangu, dhahabu na fedha yangu. Nami sikumkatalia!”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Ndipo Ahabu mfalme wa Israeli, akawaita viongozi wote wa nchi, akawaambia, “Sasa, oneni jinsi jamaa huyu anavyotaka kututaabisha! Ametuma ujumbe kwamba anataka wake zangu, watoto wangu, dhahabu na fedha yangu. Nami sikumkatalia!”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi, akawaambia, “Tazama jinsi mtu huyu anavyochochea matatizo! Alipotuma apelekewe wake zangu na watoto wangu, fedha zangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi na akawaambia, “Tazama jinsi mtu huyu anavyochokoza! Wakati alipotuma apelekewe wake zangu na watoto wangu, fedha zangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

7 Ndipo mfalme wa Israeli, akawaita wazee wote wa nchi, akasema, Angalieni, nawaomba, mwone, kwamba huyu ataka madhara; maana ametuma kwangu kutaka wake zangu na watoto wangu; na fedha yangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.

Tazama sura Nakili




1 Wafalme 20:7
18 Marejeleo ya Msalaba  

lakini kesho kama wakati huu nitatuma kwako watumwa wangu, ili wachunguze nyumba yako na nyumba za watumwa wako; na itakuwa kila kipendezacho machoni pako watakitia mikononi mwao, na kukichukua.


Wakamwambia wazee wote na watu wote, Usisikie, wala usikubali.


Basi, akaandika nyaraka kwa jina la Ahabu, akazitia mhuri wake, akazipeleka zile nyaraka kwa wazee, na kwa watu wenye nguvu waliokuwa katika mji wake, waliokaa pamoja na Nabothi.


Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa makabila na wakuu wa koo za wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la Agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.


Ikawa, mfalme wa Israeli alipousoma waraka, alirarua mavazi yake, akasema, Je! Mimi ni Mungu, niue na kuhuisha, hata mtu huyu akanipelekea mtu nimponye ukoma wake? Fahamuni, basi, nakusihini, mwone ya kuwa mtu huyu anataka kugombana nami.


Kisha Daudi akafanya shauri na makamanda wa maelfu, na makamanda wa mamia, naam, na kila kiongozi.


Kisha Daudi akawakusanya huko Yerusalemu wakuu wote wa Israeli, wakuu wa kabila, na makamanda wa vikosi wenye kumtumikia mfalme kwa zamu, na makamanda wa maelfu, na makamanda wa mamia, na wenye kutawala juu ya mali na milki za mfalme, na za wanawe, pamoja na matowashi, na mashujaa, naam, wanaume mashujaa wote.


Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Na mioyo yao hutunga udanganyifu.


Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huchochea vita.


Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.


Hadi lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama ua ulio tayari kuanguka,


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.


Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili; Atafutaye madhara, hayo yatamjia.


Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara.


Mna upotovu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.


Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo