Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Timotheo 4:15 - Swahili Revised Union Version

15 Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

15 Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.

Tazama sura Nakili




1 Timotheo 4:15
26 Marejeleo ya Msalaba  

Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.


Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Maana furaha yangu hutoka kwa BWANA.


Yakumbukeni matendo yake ya ajabu aliyoyafanya, Miujiza yake na hukumu alizotoa.


Nakaa macho usiku kucha, Ili kuitafakari ahadi yako.


Nitayatafakari maagizo yako, Na kuziangalia njia zako.


Wakuu nao waliketi wakaninena, Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.


Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako.


Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.


Ninazo akili kuliko waalimu wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.


Nimezikumbuka siku za kale, Nimeyatafakari matendo yako yote, Naziwaza kazi za mikono yako.


Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.


Kinywa changu kitanena hekima, Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara.


Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Ninakutafakari usiku kucha.


Pia nitaitafakari kazi yako yote; Nitaziwaza habari za matendo yako.


lakini watawasaidia na ndugu zao katika hema ya kukutania, kufanya kazi zao, lakini wasitumike katika huo utumishi tena. Ndivyo utakavyowafanyia Walawi katika mambo ya ulinzi wao.


Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.


na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.


Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumia watakatifu);


tukijua ya kwamba yeye aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi nasi pamoja na Yesu, na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.


Tena walitenda hivi si kama tulivyotumaini tu, bali kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana; na kwetu pia, kwa mapenzi ya Mungu.


Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.


Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako, na wale wakusikiao pia.


Uwakumbushe ndugu mambo hayo, nawe utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, na mzoefu wa maneno ya imani, na mafundisho mazuri yale uliyoyafuata.


ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wake mwenyewe walio na bidii katika matendo mema.


Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda kulingana na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo