Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yoeli 1:4 - Swahili Revised Union Version

Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nzige, makundi kwa makundi, wameivamia mimea; kilichoachwa na nzige kimeliwa na tunutu, kilichoachwa na tunutu kimeliwa na parare, kilichoachwa na parare kimeliwa na matumatu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nzige, makundi kwa makundi, wameivamia mimea; kilichoachwa na nzige kimeliwa na tunutu, kilichoachwa na tunutu kimeliwa na parare, kilichoachwa na parare kimeliwa na matumatu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nzige, makundi kwa makundi, wameivamia mimea; kilichoachwa na nzige kimeliwa na tunutu, kilichoachwa na tunutu kimeliwa na parare, kilichoachwa na parare kimeliwa na matumatu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kilichosazwa na kundi la tunutu nzige wakubwa wamekula, kilichosazwa na nzige wakubwa parare wamekula, kilichosazwa na parare madumadu wamekula.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kilichosazwa na kundi la tunutu nzige wakubwa wamekula, kilichosazwa na nzige wakubwa parare wamekula, kilichosazwa na parare madumadu wamekula.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yoeli 1:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Ikiwa kuna njaa katika nchi, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewazingira katika mji wao wowote ule; au ukiwapo msiba wowote, au ugonjwa wowote;


Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukame, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao, au ukiwapo msiba wowote, au ugonjwa wowote;


Nikizifunga mbingu isiwepo mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwatumia watu wangu tauni;


Alisema, kukaja nzige, Na tunutu wasiohesabika;


Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige matunda ya kazi yao.


Au, kwamba wakataa kuwapa hao watu wangu ruhusa waende zao, tazama, kesho nitaleta nzige waingie ndani ya mipaka yako;


nao wataufunika uso wa nchi, mtu asipate kuona hiyo nchi; nao watakula mabaki ya hayo yaliyopona yaliyowasalia baada ya ile mvua ya mawe, watakula kila mti umeao kwa ajili yenu mashambani;


Na mateka yako yatakukusanywa kama wadudu wakumbavyo, wataruka juu yake kama arukavyo nzige.


BWANA wa majeshi ameapa kwa nafsi yake, akisema, Hakika nitakujaza watu, kama nzige, nao watapiga kelele juu yako.


Itwekeni bendera katika nchi, pigeni tarumbeta kati ya mataifa, yawekeni mataifa tayari juu yake; ziiteni juu yake falme za Ararati, na Mini, na Ashkenazi; agizeni jemadari juu yake; wapandisheni farasi, kama tunutu.


Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.


Nami nimewapiga kwa ukame na kuvu; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema BWANA.


Haya ndiyo aliyonionesha Bwana MUNGU; tazama, aliumba nzige mwanzo wa kuchipuka kwake mimea wakati wa vuli; na tazama, ilikuwa mimea ya wakati wa vuli baada ya mavuno ya mfalme.


Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi.


Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila.


Miti yako yote, na mazao ya nchi yako, nzige watakuwa nayo.