Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Walawi 11:7 - Swahili Revised Union Version

Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Walawi 11:7
11 Marejeleo ya Msalaba  

waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;


Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA.


Yeye achinjaye ng'ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.


Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu iliyopasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.


Na sungura, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.


Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu.


Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.


Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.


Pepo wakamtoka mtu yule wakawaingia nguruwe, nalo kundi liliteremka gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa maji.


na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.