Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wafilipi 2:5 - Swahili Revised Union Version

Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Muwe na msimamo uleule aliokuwa nao Kristo Yesu:

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Muwe na msimamo uleule aliokuwa nao Kristo Yesu:

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Muwe na msimamo uleule aliokuwa nao Kristo Yesu:

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kuweni na nia ile ile aliyokuwa nayo Al-Masihi Isa:

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kuweni na nia ile ile aliyokuwa nayo Al-Masihi Isa:

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Iweni na nia hiyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wafilipi 2:5
16 Marejeleo ya Msalaba  

Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;


Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.


habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huku na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


Na ndugu yako akichukizwa kwa sababu ya chakula, umeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula chako usimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.


Kwa maana Kristo naye hakujipendeza mwenyewe; bali kama ilivyoandikwa, Matusi yao waliokutusi wewe yalinipata mimi.


Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunuia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa kufuata mfano wa Kristo Yesu;


vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.


mkaende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.


Paulo na Timotheo, watumwa wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu, walioko Filipi, pamoja na maaskofu na mashemasi.


Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.


Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.


Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.