Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Wafilipi 1:21 - Swahili Revised Union Version

Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwangu, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida zaidi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwangu, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida zaidi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwangu, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida zaidi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Al-Masihi, na kufa ni faida.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Al-Masihi, na kufa ni faida.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Wafilipi 1:21
16 Marejeleo ya Msalaba  

Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;


kwamba ni Paulo, au Apolo, au Kefa; au dunia, au uzima, au mauti; au vile vilivyopo sasa, au vile vitakavyokuwapo; vyote ni vyenu;


Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.


Basi siku zote tuna moyo mkuu; tena twajua ya kuwa, wakati tuwapo hapa katika mwili, tunakaa mbali na Bwana.


Lakini tuna moyo mkuu; nasi tunaona ni afadhali kutokuwemo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana.


Nimesulubiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.


Lakini mimi, la hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulubishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.


kama vile nilivyotazamia sana, na kutumaini, kwamba sitaaibika kamwe, bali kwa uthabiti wote, kama sikuzote na sasa vivyo hivyo Kristo ataadhimishwa katika mwili wangu; ikiwa kwa maisha yangu, au ikiwa kwa mauti yangu.


Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.


Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;


Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.


Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu.


Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.