Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Nahumu 2:1 - Swahili Revised Union Version

Yeye apondaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwangamizi amekuja kukushambulia ee Ninewi. Chunga ngome zako! Weka ulinzi barabarani! Jiweke tayari! Kusanya nguvu zako zote!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwangamizi amekuja kukushambulia ee Ninewi. Chunga ngome zako! Weka ulinzi barabarani! Jiweke tayari! Kusanya nguvu zako zote!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwangamizi amekuja kukushambulia ee Ninewi. Chunga ngome zako! Weka ulinzi barabarani! Jiweke tayari! Kusanya nguvu zako zote!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi. Linda ngome yako, chunga barabara, jitieni nguvu wenyewe, kusanya nguvu zako zote!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mshambuliaji anasogea dhidi yako, Ninawi. Linda ngome, chunga barabara, jitieni nguvu wenyewe, kusanya nguvu zako zote!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye apondaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Nahumu 2:1
14 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini ukitaka kwenda, haya, jitie nguvu upigane; Mungu atakuangusha mbele ya adui; maana Mungu anazo nguvu za kusaidia, na kuangusha.


Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye Juu nadhiri zako.


Wewe usikiaye maombi, Wote wenye mwili watakujia.


Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu.


Na wingi wa mataifa wapiganao na Arieli, wote wapiganao naye na ngome yake, na wanaomwudhi, watakuwa kama ndoto, na maono ya usiku.


Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni.


Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima Miguu yake aletaye habari njema, Yeye aitangazaye amani, Aletaye habari njema ya mambo mema, Yeye autangazaye wokovu, Auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!


angalieni, nitatuma watu na kuzitwaa jamaa zote za upande wa kaskazini, asema BWANA, nami nitatuma ujumbe kwa Nebukadneza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitawaleta juu ya nchi hii, na juu yao wakaao ndani yake, na juu ya mataifa haya yote yaliyoko pande zote; nami nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kitu cha kushangaza, na kitu cha kuzomewa, na ukiwa wa daima.


Imekuwaje nyundo ya dunia yote Kukatiliwa mbali na kuvunjwa? Imekuwaje Babeli kuwa ukiwa Katikati ya mataifa?