Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 14:6 - Swahili Revised Union Version

6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 ambayo kwa hasira waliyapiga mataifa kwa mapigo yasiyo na kikomo, nao kwa ghadhabu kali waliwatiisha mataifa kwa jeuri pasipo huruma.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 ambayo kwa hasira waliyapiga mataifa kwa mapigo yasiyo na kikomo, nao kwa ghadhabu kali waliwatiisha mataifa kwa jeuri pasipo huruma.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu.

Tazama sura Nakili




Isaya 14:6
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mnyonge; akawatia wote mkononi mwake.


Mungu haondoi hasira zake; Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.


Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya BWANA.


Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.


Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama katika kiota cha ndege; na kama vile watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya dunia yote; wala hapana aliyetikisa bawa, wala kufumbua kinywa, wala kulia.


BWANA amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.


Ole wako uharibuye ila hukuharibiwa, utendaye hila wala hukutendwa hila! Utakapokwisha kuharibu, utaharibiwa wewe; na utakapokwisha kutenda kwa hila, wao watakutenda hila wewe.


na wafalme wote wa kaskazini, walio mbali na walio karibu, wote pamoja; na falme zote za dunia, zilizoko katika dunia; na mfalme wa Sheshaki atakunywa baada yao.


angalieni, nitatuma watu na kuzitwaa jamaa zote za upande wa kaskazini, asema BWANA, nami nitatuma ujumbe kwa Nebukadneza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitawaleta juu ya nchi hii, na juu yao wakaao ndani yake, na juu ya mataifa haya yote yaliyoko pande zote; nami nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kitu cha kushangaza, na kitu cha kuzomewa, na ukiwa wa daima.


Ninyi nyote mnaomzunguka, mlilieni, Nanyi nyote mlijuao jina lake, semeni, Jinsi ilivyovunjika fimbo ya enzi, Fimbo ile iliyokuwa nzuri!


Tazama, mimi ni juu yako, Ewe mwenye kiburi, asema Bwana, BWANA wa majeshi; maana siku yako imewadia, wakati nitakapokujia.


Wamesikia kwamba napiga kite; Hakuna hata mmoja wa kunifariji; Adui zangu wote wamesikia habari ya mashaka yaliyonipata; Hufurahi kwa kuwa umeyafanya hayo; Utaileta siku ile uliyoitangaza, Nao watakuwa kama mimi.


na watu wote wanaokaa duniani wamehesabiwa kuwa si kitu, naye hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, Unafanya nini wewe?


Je! Atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima?


Naam, pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu chungu.


Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo