Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 32:16 - Swahili Revised Union Version

Akawatia mkononi mwa watumwa wake, kila kundi peke yake. Naye akawaambia watumwa wake, Vukeni mbele yangu, mkaache nafasi kati ya kundi na kundi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Akawakabidhi watumishi wake, kila mmoja kundi lake, akawaambia, “Nitangulieni mkiacha nafasi kati ya kundi na kundi katika msafara wenu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Akawakabidhi watumishi wake, kila mmoja kundi lake, akawaambia, “Nitangulieni mkiacha nafasi kati ya kundi na kundi katika msafara wenu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Akawakabidhi watumishi wake, kila mmoja kundi lake, akawaambia, “Nitangulieni mkiacha nafasi kati ya kundi na kundi katika msafara wenu.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake, na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Akaviweka chini ya uangalizi wa watumishi wake, kila kundi peke yake na kuwaambia, “Nitangulieni na kuacha nafasi kati ya makundi.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akawatia mkononi mwa watumwa wake, kila kundi peke yake. Naye akawaambia watumwa wake, Vukeni mbele yangu, mkaache nafasi kati ya kundi na kundi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 32:16
9 Marejeleo ya Msalaba  

ngamia wanyonyeshao thelathini pamoja na wana wao, ng'ombe majike arubaini na mafahali kumi; punda wake ishirini na wana wao kumi.


Akamwagiza yule wa kwanza akasema, Esau, ndugu yangu, akikukuta, na kukuuliza, akisema, Wewe ni wa nani? Unakwenda wapi? Tena ni wa nani hawa walio mbele yako?


Tena semeni, Tazama, mtumwa wako, Yakobo, yuko nyuma yetu. Maana alisema, Nitamsuluhisha kwa zawadi inayonitangulia, baadaye nitamwona uso wake; huenda atanikubali uso wangu.


Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.


Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi.


Kwa maana Mungu wake anamwagiza vizuri na kumfundisha.


Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwamwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.


Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.