Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mika 7:11 - Swahili Revised Union Version

Ni siku ya kujengwa kuta zako! Siku hiyo mpaka utasongezwa mbali.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Siku yaja ambapo kuta za mji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya nchi yenu itapanuliwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Siku yaja ambapo kuta za mji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya nchi yenu itapanuliwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Siku yaja ambapo kuta za mji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya nchi yenu itapanuliwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ni siku ya kujengwa kuta zako! Siku hiyo mpaka utasongezwa mbali.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mika 7:11
12 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha nikawaambia, Mnaona hali hii dhaifu tuliyo nayo, jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa, na malango yake yalivyoteketezwa kwa moto; haya! Na tuujenge tena ukuta wa Yerusalemu, ili tusiwe shutumu tena.


nipewe na waraka kwa Asafu, mwenye kuutunza msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengenezea boriti kwa malango ya ngome ya hekalu, na kwa ukuta wa mji; na kwa nyumba ile nitakapoishi mimi. Naye mfalme akanipa, maana mkono mwema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu.


Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema, Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe.


Basi tukaujenga ukuta; nao ukuta wote ukaunganishwa kiasi cha nusu ya kimo chake; maana watu walikuwa na moyo wa kufanya kazi.


Ewe uliyeteswa, uliyerushwa na tufani, usiyetulizwa, tazama, nitaweka mawe yako kwa rangi nzuri, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.


Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako.


Na watu wako watapajenga mahali palipokuwa ukiwa; utaiinua misingi ya vizazi vingi; nawe utaitwa, Mwenye kutengeneza mahali palipobomoka; na, Mwenye kurejesha njia za kukaa.


Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.


Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu.