Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:22 - Swahili Revised Union Version

Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi, huruma zake hazina mwisho.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi, huruma zake hazina mwisho.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi, huruma zake hazina mwisho.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa sababu ya upendo mkuu wa Mwenyezi Mungu, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa sababu ya upendo mkuu wa bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:22
20 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na tuanguke katika mkono wa BWANA; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.


Ila kwa rehema zako nyingi hukuwakomesha kabisa, wala kuwaacha; kwa maana wewe u Mungu mwenye neema na rehema.


Hakututenda kulingana na hatia zetu, Wala hakutulipa kwa kadiri ya maovu yetu.


Akawakumbukia agano lake; Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;


Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.


Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?


Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.


Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.


Nenda, ukatangaze maneno haya kuelekea upande wa kaskazini, ukaseme, Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi, asema BWANA; sitakutazama kwa hasira; maana mimi ni mwenye rehema, asema BWANA, sitashika hasira hata milele.


Maana mimi ni pamoja nawe, asema BWANA, nikuokoe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokutawanya, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu.


Je! Efraimu siye mwanangu mpendwa? Je! Siye mtoto apendezaye? Maana kila nisemapo neno juu yake, ningali nikimkumbuka sana; kwa sababu hiyo moyo wangu unataabika kwa ajili yake; bila shaka nitamrehemu, asema BWANA.


Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi;


Kwa kuwa mimi, BWANA, sina kigeugeu; ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.


Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.