Maombolezo 3:1 - Swahili Revised Union Version Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Mimi ni mtu niliyepata mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake Mungu. Biblia Habari Njema - BHND Mimi ni mtu niliyepata mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake Mungu. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Mimi ni mtu niliyepata mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake Mungu. Neno: Bibilia Takatifu Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake. Neno: Maandiko Matakatifu Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake. BIBLIA KISWAHILI Mimi ni mtu niliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake. |
Wewe, uliyetuonesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Kutoka katika vina virefu chini ya nchi.
Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Basi wakamtwaa Yeremia, wakamtupa katika shimo la Malkiya, mwana wa mfalme, lililo katika ukumbi wa walinzi; wakamshusha kwa kamba. Na mle shimoni hamkuwa na maji, ila matope tu; naye Yeremia akazama katika matope hayo.
wanaume, na wanawake, na watoto, na binti za mfalme, na kila mtu ambaye Nebuzaradani, mkuu wa askari walinzi, amemwacha pamoja na Gedalia, mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, pia na Yeremia, nabii, na Baruku, mwana wa Neria;
Kwa sababu ya maumivu ya binti ya watu wangu nimeumia mimi; nimevaa kaniki; ushangao umenishika.