Ndipo Asa akamkasirikia mwonaji, akamtia katika nyumba ya magandalo gerezani, maana amemghadhibikia kwa sababu ya neno hilo. Na wakati uleule Asa akatesa baadhi ya watu.
Luka 4:28 - Swahili Revised Union Version Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana. Biblia Habari Njema - BHND Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana. Neno: Bibilia Takatifu Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana. Neno: Maandiko Matakatifu Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana. BIBLIA KISWAHILI Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo. |
Ndipo Asa akamkasirikia mwonaji, akamtia katika nyumba ya magandalo gerezani, maana amemghadhibikia kwa sababu ya neno hilo. Na wakati uleule Asa akatesa baadhi ya watu.
Basi wakamtwaa Yeremia, wakamtupa katika shimo la Malkiya, mwana wa mfalme, lililo katika ukumbi wa walinzi; wakamshusha kwa kamba. Na mle shimoni hamkuwa na maji, ila matope tu; naye Yeremia akazama katika matope hayo.
Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale majusi, alighadhibika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wa kiume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake kote, kuanzia wenye miaka miwili na chini yake, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale majusi.
Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.
Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini;